KABLA YA KUANZISHA BIASHARA YAKO HAKIKISHA UNA SIFA ZIFUATAZO:
Nidhamu
binafsi – Hakuna mjasiriamali anayependa kuona
biashara yake inakufa, kila mmoja analenga kuhakikisha biashara inafanikiwa na
huondosha kila jambo linaloweza kuhatarisha ustawi wa biashara husika.
Wajasiriamali waliofanikiwa wana nidhamu ya kuchukua hatua kila siku kuelekea
kwenye kufanikisha malengo yao. Hakikisha unanidhamu ya kutunza mda na nidhamu
ya kutumia pesa zinazopatikana kutokana na biashara yako.
Kujiamini –
Mjasiriamali hupaswi kuwa na wasiwasi kuwa unaweza kufanikiwa au la, unapaswa
kujiamini mda wote kuwa utafanikisha biashara yako. Jitahidi kudhihirisha
kujiamini huko kwa kufanya kazi kwa bidii ili kifikia malengo uliyojiwekea.
Muwazi wa
fikra – Mjasiriamali anatambua kuwa kila tukio au
hali ni fursa ya kibiashara. Mawazo mapya yanaibuliwa kila mara kuhusu
mtiririko wa kazi na ufanisi, ujuzi, na biashara mpya. Mjasiriamali ana uwezo
wa kutizama kila jambo [hali/ tukio] linalomzunguka na kulitumia kufanikisha
lengo lake.
Muanzilishi – Mjasiriamali anafahamu kuwa
kama kuna jambo linalopaswa kufanyika basi yeye mwenyewe ndiye anayepaswa
kulianzisha. Hujiwekea vigezo na kuhakikisha biashara inafuata kuelekea
kutekeleza/ kukidhi vigezo hivyo. Wako makini katika kutwaa fursa bila kuhitaji
kusubiri mtu mwingine awape fursa
Mshindani –
Chanzo cha biashara nyingi ni mjasiriamali mmoja kutambua kuwa anaweza kufanya
biashara hiyo kwa ubora kuliko mwingine/ wengine. Wajasiriamali wanahitaji
kufanikiwa katika biashara wanazoanzisha mithili ya mchezaji anavyohitaji
kushinda katika mchezo anaocheza. Mjasiriamali ni mwepesi kuonesha namna
taasisi yake ilivyofanikiwa katika hatua mbalimbali.
Mbunifu –
mojawapo ya mambo muhimu katika ubunifu ni kumudu kuunganisha mambo ambayo
hayaonekani kuwa na uhusiano katika kutengeneza fursa. Wajasiriamali huja na
suluhisho baada ya kuchambua na kutengeneza uhusiano wa hali/ matukio
mbalimbali. Huweza hata kubadili malengo ya bidhaa fulani na kuiuza katika soko
tofauti.
Kutokata tamaa – Wajasiriamali hawakatishwi tamaa na kushindwa. Kila anaposhidwa
huichukulia kama fursa ya kujifunza na kufanikiwa. Wanatamani kila wanalofanya
lifanikiwe, hivyo hujaribu tena na tena hadi wafanikiwe. Hawaamini kuwa kuna
jambo lisilowezekana
Ujuzi binafsi – Mjasiriamali ana ujuzi mzuri wa kuwasiliana katika kuuza na
kuwapa motisha waajiriwa wao. Wajasiriamali wengi waliofanikiwa hufahamu namna
ya kuwapa motisha waajiriwa wao hivyo kukuza biashara zao. Ni wazuri katika
kuelezea faida za hali mbalimbali na kuwafundisha wengine katika kufanikiwa.
Mwenye
kuheshimu maadili ya kazi yake – Mjasiriamali hufanikiwa kwa kufuata/ kutii kanuni na taratibu
zilizowekwa na mamlaka husika. Mifano ya wajasiriamali wasio na maadili ni:
Muuzaji wa matunda anayeokota matunda kutoka kwenye shimo la taka kwa ajili ya
kuwatengenezea wateja wake sharubati (juisi), au mjasiriamali anayeuza nyama
isiyokaguliwa au iliyokatazwa kwa matumizi ya binadamu.
Mwenye
kupenda kazi yake – Kupenda na kuthamini kazi
yake ni sifa muhimu kuliko zote anayohitaji mjasiriamali ili kufanikiwa.
Mjasiriamali ana mapenzi ya dhati kwa kazi yake. Yuko tayari kufanya kazi saa
za ziada kuhakikisha biashara yake inafanikiwa, maana hupata furaha kuona
biashara inafanikiwa. Mjasiriamali anayefanikiwa ni yule ambaye hujifunza bila
kuchoka na kutafiti namna mbalimbali za kufanya biashara yake iwe bora zaidi.
Wajasiriamali wanaofanikiwa
hutizama biashara zao kama mtu aliye juu ya kilima na kuona biashara yake
ilivyo. Akishaiona, anataka kwenda mbali zaidi. Wanafahamu namna ya kuzungumza
na waajiriwa wao, na biashara zao hutanuka kwa sababu hiyo.
No comments:
Post a Comment